Udadisi wa Wanafunzi wa Ilboru kuhusu Jua na Nishati yake

Maswali ya udadisi hapo chini kuhusu Jua na Nishati yake yameulizwa na wanafunzi wa shule ya Msingi ilboru mkoani Arusha katika Club ya sayansi baada ya kujifunza kuhusu Nyota ya Jua. Kupitia kipindi hiko wanafunzi pia walichunguza na kulitazama jua kwa kutumia miwani maalumu ya kutazama Jua (Solar Eclipse Shade) pamoja na vifaa vingine kama Solar Prism. 

Unaweza kushirikiana kwa kujifunza pamoja na wanafunzi hawa kwa kujibu maswali hapo chini au kwa kushirikiana nao kwenye mjadala kuhusu maswali haya na mengine. Ili kufanya hivyo unaweza kuwasiliana na mwalimu wao Bwana Eliatosha Maleko kwa kupitia eliatosha@gmail.com

  1. Clara Elirehema aliuliza:

           Hapa duniani yako madini mbalimbali ambayo ni muhimu sana katika kuzalisha vitu mbalimbali, je wataalamu hawaoni umuhimu wa kutumia gesi zitokanazo na jua kama gesi ya Hydrogen ambayo ni zaidi ya asilimia 92, Hellium asilimia 83 zinazounda jua?

  1. Rebeca Abraham aliuliza:

       Je ni vifaa gani hutumika kulichunguza na kulipima jua na je, ni vifaa kutoka mataifa gani?

  1. Caren James aliuliza:

     Tunajifunza kuwa wapo wanasayansi na nchi mbalimbali duniani zilizotumia na kupeleka Satelite angani pamoja na wanasayansi katika Mwezi, Je katika nyota jua wapo wanasayansi waliowahi kwenda na je kwenye nyota jua kuna ardhi kama ilivyo duniani?.

  1. Maliki Abasi aliuliza:

    Upepo wa jua una faida gani kwa viumbe hai au madhara gani ikiwa utafika duniani?.

  1. Neema Florence aliuza:

Tumejifunza kuwa umri wa nyota jua ni miaka Bilioni 4 na nusu, Je umri wa jua unapimwaje ? Na je, jua linazeeka au kupunguza mwanga wake au nguvu yake kuanzia lilipoumbwa?

  1. Noela Erick aliuliza:

     Katika masomo ya Jiografia na Sayansi tumejifunza kuwa Nishati huweza kuhifadhiwa kwa muda mrefu, Je mataifa duniani mwote  hayaoni umuhimu wa kuwa na hifadhi kubwa ya nishati itokanayo na jua kama wanavyohifadhi nishati ya mafuta kama vile Petroli, dizeli na mafuta ya taa?

  1. Aneth Aristides aliuliza:

    Nini maana ya Nuclear  fussion, na je ina umuhimu gani  katika maisha yetu ya kila siku?

  1. Emaculata Pauli aliuliza:

     Tumejifunza kwamba jua linatoa joto zaidi ya nyuzi Bilioni za joto na sehemu ya uso wake hutoa joto nyuzi 6000°C, je ni kwanini katika Viwanda vikubwa duniani havitumia joto la jua katika kuyeyusha vyuma vizito na vitu vingine   vinavyohitaji joto kubwa ili kuyeyushwa?

 Wapendwa haya ni baadhi tu ya maswali  yatokanayo na kipindi hicho  ni matumaini yetu kuwa majibu yenu yatatupatia uelewa zaidi. 

One Reply to “Udadisi wa Wanafunzi wa Ilboru kuhusu Jua na Nishati yake”

  1. Habari Eliatosha,

    Ni furaha kuona wanafunzi wako wanazidi kuwa wadadisi siku hadi siku na kuona jinsi wanavyouliza maswali ya kufikirika zaidi.

    Haya ni mawazo yangu juu ya baadhi ya maswali yaliyoulizwa.

    1. Clara ametaka kujua kuhusu matumizi ya gesi zitokanazo na Jua, hili ni swali zuri ambalo hata mimi sijui jibu lake ila nafikiri tatizo tulilonalo ni namka ya kwenda kwenye Jua na kuzivuna hizo gesi.

    Nna hakika kuwa mmejifunza kuwa kwenye Jua kuna joto kali sana, na vyombo vyetu vingi haviwezi kuhimili joto hilo, hivyo kuwa na vifaa vya kuweza kuvuna hizo gesi bado ni changamoto kwetu.

    2. Nami pia nna shauku ya kujua zaidi kuhusu swali la Rebecca, nitakuwa na kuja hapa ili kupata majibu ya swali hili.

    3. Hakika swali la Caren ni zuri, ila nawaza ni kwa namna gani bindamu anaweza kuhimili joto kali la Jua, je kuna vyombo vinavyoweza kuingia kwenye Jua na kumfanya binadamu awe kama alivyo. Hadi leo sijajua kama hili linawezekana ila nimesikia kuna chombo ambacho kimetumwa kwenye Jua, labda chombo hiki kitaweza kusaidia kutupa majibu ya swali la Caren, tuendelee wote kufuatilia na kujua zaidi. Unaweza kusoma zaidi kuhusu kifaa hiki hapa https://www.bbc.com/swahili/habari-53449254

    Kuhusu swali la pili, ni wazi kuwa kwa Joto kali lilipo kwenye uso na kiini cha Jua ni vigumu kuwa na uso wa ardhi kama wa kwenye uso wa Dunia. Unaweza kujifunza zaidi kuhusu Jua kwenye tovuti hii https://sw.wikipedia.org/wiki/Jua

    4. Nami pia nna shauku ya kujua zaidi kuhusu majibu ya swali la nne, kulingana na ufahamu wangu wa sasa nahisi upepo wa Jua unaweza kusababisha muingiliano wa mawimbi ya mawasiliano na kupelekea mawasiliano kuwa ya shida kwa wakati husika.

    5. Swali hili hakika ni zuri na labda linahitaji wanasayansi wabobezi kutusaidia.

    6. Noel ameuliza swali zuri sana ambalo wanasayansi wengi wanalifanyia kazi leo hii. Kama ameshawahi kuona taa za mwanga wa Jua au solar, basi hivyo ndivyo tunavyovuna nguvu ya jua ili iwe nishati ya kutusaidia. Hata hivyo bado tuna safari ndefu ya kuvuna nishati hii inayopatikana kwa urahisi na ya uhakika zaidi. Mimea ipo mbali katika hili maana yenyewe huchukua nishati ya mwanga wa Jua na kuigeuza kuwa chakula tunachokula ili kupata nguvu.

    7. Aneth ameuliza swali zuri kuhusu nuclear fusion, hii ni njia ambayo jua hutoa mwanga na nguvu yake inayolifanya ling’ae. Bila nyuklia fusion, hakutakuwa na mwanga wa Jua na Dunia yote itakuwa giza na viumbe wote tutakufa, maana tunahitaji mwanga wa jua ili kuishi na kupata nguvu.

    8. Emaculata swali lako ni zuri na si rahisi kulijibu, ingawa kiasi cha nguvu ya Jua kinachofika Dunia ni kidogo sana kulinganisha na nguvu yake yote ya asili, hii inapekelea kushindwa kutumia nishati yote inayotolewa. Ila hata kwa kiasi kidogo kinachofika Duniani, bado tunaweza kuhifadhi baadhi ya nishati hiyo na kuitumia kuchaji simu, kuwasha taa, kuangalia TV na kusikiliza redio.

    Tuendelee kujadiliana na kujifunza pamoja, maana haya ni mawazo yangu naweza kuwa nimepatia au nimekosea. Ila hii ndio raha ya kujifunza pamoja nawe.

Leave a Reply